Main Title

source : Parstoday
Jumanne

26 Desemba 2023

17:10:53
1423949

Ujumbe wa kuendelea maandamano ya wananchi wa Uturuki dhidi ya Israel

Licha za siasa za kundumakuwili za serikali ya Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki kuhusu masuala ya Palestina, wananchi wa nchi hiyo bado wanaendelea na maandamano yao ya kihamasa dhidi ya Israeli.

Kuhusiana na jambo hilo, wananchi wa Uturuki walifanya maandamano makubwa karibuni mjini Ankara ikiwa ni katika kulaani mauaji ya kimbari huko Palestina, mashambulizi ya mara kwa mara ya utawala wa kibaguzi wa Israel dhidi ya raia wa Gaza na pia kuunga mkono taifa la Palestina. Maandamano hayo, ambayo yaliandaliwa na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali huko Ankara, yalianzia katika kituo cha metro cha Atatürk na kumalizikia kwa taarifa ya pamoja ya kutetea Gaza katika uwanja wa Anadolu.

Washiriki wa Maandamano Makubwa ya Gaza katika mji mkuu wa Uturuki, kwanza walitoa heshima zao kwa waandishi wa habari ambao waliuawa shahidi katika mashambulizi ya utawala wa kibaguzi wa Israel huko Gaza. Tokea tarehe 7 Novemba hadi sasa zaidi ya Wapalestina elfu 20 na 500 wameuawa shahidi katika Ukanda wa Gaza. Takwimu za mauaji ya kimbari na ya kizazi dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina zinaonyesha kiwango cha jinai zinazotekelezwa na utawala katili wa Kizayuni huko Gaza. Katika hali hiyo ni wazi kuwa, nchi nyingine duniani ikiwemo Marekani na waitifaki wake bado zinaendeleza uungaji mkono wao kwa jinai hizo za Israel huko Gaza.

342/