Kesho Jumamosi, ni siku ya kuadhimisha kumbukumbu ya Hamasa ya tarehe 9 Dey. Tarehe 9 Dey 1388 inayosadifiana na Desemba 30, 2009 inakumbusha maandamano yaliyofanywa na mamilioni ya wananchi wa Iran kutangaza kujibari na kujitenga na wavurugaji nidhamu ya jamii na kutoa jibu madhubuti pia kwa wazushaji fitna, walioamua kufuata njia pogo na isiyo sahihi kwa kisingizio cha kufanyika udanganyifu katika uchaguzi wa kumi wa rais wa Iran. Hamasa ya Dey 9 ni nembo ya heshima, uhuru na basira ya wananchi wa Iran, ambao walisimama imara hata kwa gharama ya kutoa mhanga roho zao kwa ajili ya kulinda usuli na misingi ya Uislamu na malengo matukufu ya Mapinduzi na kupaza sauti zao kwamba ikiwa maadui watasimama dhidi ya dini yao, na wao watasimama dhidi ya ulimwengu wao wote. Kwa mnasaba huo na kwa mujibu wa IRNA, Hujjatul-Islam wal-Muslimin Mohammad Javad Haj Ali Akbari amesema katika khutba za Sala ya Ijumaa ya wiki hii hapa Tehran ya kwamba: "hatua makini na subira ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi na kujitokeza kikamilifu wananchi tarehe 9 Dey kuliiokoa Iran na fitna hiyo hatari; kwa hivyo, lazima tuidumishe siku hii na tuwafungie njia wafanya fitna kwa basira na urazini".Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran ameongeza kuwa: "kilichotokea wakati wa fitna ya Marekani ya mwaka 88 Hijria Shamsia ni uadui uliokuwa umepangwa na kuratibiwa na maadui walioikamia Iran ya kwamba, kama hawatafanikiwa kabla ya uchaguzi, wachukue hatua baada ya uchaguzi; na ndio kama mlivyoona, katika mwaka 88 ilitokea fitna hatari zaidi kuwahi kushuhudiwa tokea Mapinduzi".
source : Parstoday
Ijumaa
29 Desemba 2023
18:19:16
1424805
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Mohammad Javad Haj Ali Akbari, Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesisitiza kudumishwa na kuendelezwa kumbukumbu ya Hamasa ya tarehe 9 Dey.