Katika taarifa yake iliyotolewa Ijumaa na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu OHCHR jijini Geneva Uswisi, Rehman amesema wale wote waliohusika na mashambulizi mabaya yaliyotokea siku ya Jumatano nchini Iran na kuua zaidi ya watu 89 lazima wawajibishwe.
Afisa huyo wa Umoja wa Mataifa amesema: “Mauaji ni mojawapo ya mashambulizi makubwa zaidi dhidi ya maadili ya kimataifa ya haki za binadamu." Aidha ametuma salamu za rambirambi na pole kwa familia za wahanga na wananchi wa Iran.
342/