Main Title

source : Parstoday
Jumapili

7 Januari 2024

18:19:25
1427474

Kamanda Qaani amhutubu Haniya: Vikosi vya Muqawama vitakuwa jinamizi kwa utawala wa Kizayuni muuaji wa watoto

Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema, vikosi vya Muqawama vitageuka kuwa jinamizi kwa utawala wa Kizayuni muuaji wa watoto.

Brigedia Jenerali Esmail Qaani ameyasema hayo katika ujumbe aliomtumia Ismail Haniya, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS kwa mnasaba wa kuuawa shahidi Saleh Al-Aouri, Naibu Mkuu wa ofisi hiyo ya kisiasa ya Hamas.Al-Arouri aliuawa shahidi katika shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala wa Kizayuni siku ya Jumanne katika viunga vya kusini mwa Beirut, mji mkuu wa Lebanon.Katika ujumbe wake huo kwa Haniya, Brigedia Jenerali Qaani, ametoa salamu za rambirambi kwa kuuawa shahidi Saleh al-Arouri na kueleza kuwa, adui Mzayuni anataka kupunguza uchungu wa kushindwa vibaya katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi kwa kuwauwa viongozi wa Muqawama.Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameongeza kuwa: Shahidi Al-Arouri aliuawa shahidi huku adui akikabiliwa na hali ngumu katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Al-Arouri ni mmoja wa waanzilishi wa Brigedi za Shahidi Izzuddin Al-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Hamas, ambapo katika kipindi cha kati ya mwaka 1991-1992 alichukua hatua ya kuasisi kikosi cha kwanza cha tawi hilo la kijeshi la Hamas katika Ukingo wa Magharibi.Mwaka 1992, jeshi la utawala wa Kizayuni lilimkamata al-Arouri na kumhukumu kifungo cha miaka 15 jela kwa kosa la kuunda kikosi cha kwanza cha Brigedi za Al-Qassam katika Ukingo wa Magharibi.

 Al-Arouri aliachiliwa kutoka jela mwaka 2007, lakini baada ya miezi mitatu utawala wa Kizayuni ulimkamata tena na kumweka gerezani.Al-Arouri alibakia katika jela za utawala haramu wa Israel kwa muda wa miaka mitatu mingine hadi mwaka 2010, wakati Mahakama ya Juu ya utawala huo ilipotoa amri ya kuachiwa huru na kubaidishwa kutoka Palestina. Wakati huo, Shahidi huyo wa Muqawama alihamishiwa Syria na kukaa katika nchi hiyo kwa miaka mitatu, kisha akapelekwa Lebanon.Mnamo mwaka 2010, baada ya kuachiliwa kutoka jela za utawala wa Israel, Shahidi Al-Arouri alichaguliwa kuwa mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya Hamas.Mnamo tarehe 9 Oktoba 2017, harakati ya Hamas ilitangaza kuwa imemchagua Saleh al-Arouri kuwa Naibu Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya harakati hiyo.../

342/