Kwa mujibu wa gazeti la Wall Street, katika ripoti yao ya siri, mashirika ya kiintelijensia ya Marekani yaliyoangazia uthabiti wa Hamas katika miezi iliyopita yamesema vita vya Israel vimeua asilimia 20 hadi 30 tu ya wanachama wa harakati hiyo ya Muqawama.
Maafisa wa Marekani ambao wamethibitisha kutolewa kwa ripoti hiyo na kusema: "Hamas ingali ina silaha za kutosha kuweza kuendelea kushambulia Israel na vikosi vya Israel huko Gaza kwa miezi kadhaa, na kundi hilo linajaribu kuunda upya jeshi lake la polisi katika maeneo ya mji wa Gaza".
Ripoti hiyo imeendelea kufichua kwamba, maafisa wenyewe wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel wamekiri kwamba hawajafikia lengo lao la kuiangamiza Hamas licha ya kuua maelfu ya raia katika mashambulio ya kinyama ya anga na ardhini yaliyofanywa na jeshi lake huko Gaza.
342/