Main Title

source : Parstoday
Ijumaa

26 Januari 2024

15:48:32
1432559

Tangazo la Marekani la kuwa tayari kwa mazungumzo ya kuhitimisha kuwepo kwake kijeshi nchini Iraq

Afisa mmoja wa Marekani ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema, katika barua ambayo balozi wa Marekani mjini Baghdad, Alina Romanovsky aliiwasilisha siku ya Jumatano kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq Fuad Hossein, Washington imetangaza kuwa iko tayari kuanza mazungumzo na Baghdad ya kuhitimisha uwepo kijeshi wa nchi hiyo na washirika wake katika ardhi ya Iraq.

Wakati malalamiko na upinzani dhidi ya kuendelea kuwepo askari 2,500 wa Marekani waliopiga kambi nchini Iraq yakiwa yamezidi kuongezeka, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq ametangaza kuwa barua ya balozi wa Marekani mjini Baghdad itashughulikiwa na Waziri Mkuu Mohammad Shia al-Sudani na maafisa husika. Afisa mmoja wa Marekani ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema pia kuwa, suala hilo si geni, na tokea huko nyuma yameshawahi kufanyika mazungumzo ya kujadili kadhia hiyo kati ya maafisa wa nchi mbili za Iraq na Marekani na akaongeza kuwa, kuanza kwa mazungumzo hayo kulishajadiliwa tangu miezi kadhaa nyuma. Afisa huyo wa Washington ameendelea kueleza kwamba, katika kipindi chote cha kufanyika mazungumzo hayo, Marekani itaendelea pia kulinda haki yake kamili ya kujihami kijeshi. 

Pamoja na hayo, nukta ya kutatanisha hapa ni kwamba siku kadhaa nyuma, yaani tarehe 16 Januari, wakati vituo vya kijeshi vya Marekani vilivyoko Iraq na Syria viliposhambuliwa, Washington ilitangaza kwamba, inakusudia kutuma wanajeshi wengine wapya 1,500 huko Iraq na Syria kutoka kikosi chake cha gadi ya taifa cha New Jersey kwa ajili ya kile ilichokiita, kupambana na kundi la kigaidi la DAESH (ISIS).

Viongozi wa Iraq wameshatoa matamko mara kadhaa ya kutaka wanajeshi wa Marekani waondoke nchini humo. Miongoni mwa viongozi hao ni Waziri Mkuu Mohammad Shia Al-Sudani, ambaye mapema Januari 2024, alisisitiza kwa mara nyingine tena wanajeshi wa Marekani waondoke haraka katika ardhi ya Iraq.

Baada ya mauaji ya kikatili ya Shahidi Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, na Shahidi Abu Mahdi al-Muhandis, Naibu wa Kikosi cha Al-Hashdu-Shaabi pamoja na waliofuatana nao yaliyofanywa na jeshi la kigaidi la Marekani karibu na uwanja wa ndege wa Baghdad mnamo Januari 3, 2020, siku mbili baadaye, yaani tarehe 5 Januari bunge la Iraq lilipiga kura kutaka vikosi vya muungano wa kupambana na DAESH vikiwemo vya Marekani viondoke katika ardhi ya nchi hiyo.

Hata hivyo Washington iliendeleza msimamo unaopingana na sheria kwa kushikilia wanajeshi wake waendelee kuwepo nchini Iraq. Hatimaye, kutokana na mashinikizo ya kisiasa ya ndani ya Iraq, Rais wa Marekani, Joe Biden, na Waziri Mkuu wa wakati huo wa Iraq, Mustafa Al-Kadhimi, walisaini makubaliano

katikati ya majira ya joto ya mwaka 2021 na kuahidi kwamba shughuli za kivita za vikosi vinavyoongozwa na Marekani nchini Iraq zitahitimishwa rasmi kabla ya kumalizika mwaka 2021.

Viongozi wa Iraq wameshatoa matamko mara kadhaa ya kutaka wanajeshi wa Marekani waondoke nchini humo. Miongoni mwa viongozi hao ni Waziri Mkuu Mohammad Shia Al-Sudani, ambaye mapema Januari 2024, alisisitiza kwa mara nyingine tena wanajeshi wa Marekani waondoke haraka katika ardhi ya Iraq.

Baada ya mauaji ya kikatili ya Shahidi Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, na Shahidi Abu Mahdi al-Muhandis, Naibu wa Kikosi cha Al-Hashdu-Shaabi pamoja na waliofuatana nao yaliyofanywa na jeshi la kigaidi la Marekani karibu na uwanja wa ndege wa Baghdad mnamo Januari 3, 2020, siku mbili baadaye, yaani tarehe 5 Januari bunge la Iraq lilipiga kura kutaka vikosi vya muungano wa kupambana na DAESH vikiwemo vya Marekani viondoke katika ardhi ya nchi hiyo.

Hata hivyo Washington iliendeleza msimamo unaopingana na sheria kwa kushikilia wanajeshi wake waendelee kuwepo nchini Iraq. Hatimaye, kutokana na mashinikizo ya kisiasa ya ndani ya Iraq, Rais wa Marekani, Joe Biden, na Waziri Mkuu wa wakati huo wa Iraq, Mustafa Al-Kadhimi, walisaini makubaliano

katikati ya majira ya joto ya mwaka 2021 na kuahidi kwamba shughuli za kivita za vikosi vinavyoongozwa na Marekani nchini Iraq zitahitimishwa rasmi kabla ya kumalizika mwaka 2021.

342/