Main Title

source : Parstoday
Jumamosi

3 Februari 2024

19:37:49
1434897

Mahakama ya Kosovo yamhukumu raia wa Serbia miaka 13 jela kwa uhalifu wa kivita

Mahakama ya Kosovo jana Ijumaa ilimhukumu raia wa Serbia aliyejulikana kwa jina la Dusko Arsic kifungo cha miaka 13 jela kwa uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na kuhusika katika unyanyasaji, kuwafukuza na kuwaua raia wa Albania huko Pristina wakati wa Vita vya Kosovo kuanzia mwaka 1998 hadi 1999.

Mahakama ya mwanzo ya Pristina imempata na hatia Dusko Arsic kwa hatua yake ya kuwalazimisha raia kuondoka Pristina na katika maeneo ya kandokando yake kati ya Januari na Juni mwaka 1999. 

Kulingana na uamuzi huo, Dusko Arsic pamoja na polisi kadhaa wa Serbia na vikundi vya wanamgambo walipora na kuharibu mali za raia wa Albania.

Arsic alitiwa mbaroni mwezi Disemba mwaka jana na alishtakiwa kwa kuhusika katika mauaji, udhalilishaji wa kingono na kisaikolojia wa raia wa Albania katika kijiji cha Butovic huko Pristina.

Wakili anayemtetea Arsic amesema atakata rufaa dhidi ya hukumu hiyo. 

342/