Vassily Nebenzia, Balozi wa Kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa amesema katika mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa, "Kwa mara nyingine tena, mashambulio hayo ya mabomu yamedhihirisha dhati ya sera za kiuhasama za Marekani Mashariki ya Kati (Asia Magharibi) na mapuuza ya Washington kwa sheria za kimataifa."
Mwanadipomasia huyo wa ngazi ya juu wa Russia amebainisha kuwa: Marekani 'inamimina mafuta' kwenye moto, kwa kufanya hujuma za anga zenye hatari ya moja kwa moja kwa amani na usalama wa dunia, mbali na kudunisha jukumu kuu la Umoja wa Mataifa."
Wakati huo huo, Zhang Jun, Balozi wa China katika Umoja wa Mataifa amekosoa vikali pia mashambulizi hayo yanayoendelea kufanywa na Marekani na Uingereza katika nchi za Iran na Syria.
342/