Kwa mujibu wa shirika la habari la FARS, Hossein Amir Abdollahian, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameonana na karibu viongozi 15 wa makundi mbalimbali ya muqawama wa Palestina mjini Damascus Syria na kujadiliana nao masuala tofauti.
Viongozi wa makundi ya mapambano ya Palestina walioshiriki kwenye mazungumzo hayo wameishukuru Jamhuri ya Kiislamu kwa uungaji mkono wake mkubwa wa taifa na kadhia ya Palestina na kuongeza kuwa, vita vya hivi sasa vya Ghaza havitokuwa vya mwisho dhidi ya utawala wa Kizayuni.
342/