Main Title

source : Parstoday
Jumapili

25 Februari 2024

17:21:43
1440266

Kufufuka uhusiano wa Iran na Sudan kwaitia wahka mkubwa Marekani

John Godfrey, balozi wa Marekani nchini Sudan, amesema katika taarifa ya uingiliaji wa wazi wa mambo yasiyomuhusu ndewe wala sikio kwamba eti ana wasiwasi wa kuimarika uhusiano kati ya Iran na Sudan kwa madai kuwa uhusiano huo utaifanya Iran iisaidie kijeshi Sudan.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Fars, zaidi ya miezi minne imepita tangu nchi mbili za Iran na Sudan kutangaza kurejesha uhusiano wa kidiplomasia baina yao, hivi sasa Marekani na baadhi ya duru zinaingilia mara kwa mara uhusiano huo kwa visingizio mbalimbali.

Katika tukio la hivi karibuni kabisa, John Godfrey, balozi wa Marekani nchini Sudan amesema katika mahojiano na waandishi wa habari kwamba: "Kuna ripoti za kuwa, kurejeshwa uhusiano kati ya Iran na Sudan kunaweza kujumuisha uungaji mkono wa kijeshi wa Iran kwa Sudan. Hili ni jambo linalotutia wasiwasi."

Amedai kuwa nchi za kigeni hazipaswi kuzipa silaha pande zinazopigana huko Sudan, wakati Marekani yenyewe ndiye muuzaji mkubwa wa silaha duniani ikiwemo kwa makundi hasimu nchini Sudan.

342/