Sheikh Uthman Husayn Taha anayejulikana zaidi kwa jina la "Uthman Taha" alikamilisha uandishi wa nakala ya Qur'ani kwa maandishi ya Naskh katika miaka ya 1970, na nakala ya Qur'ani aliyoiandika iliwavutia Waislamu wengi kwa miaka mingi.
Uthman Taha ambaye ni mzaliwa wa Syria amekuwa akiishi katika mji mtakatifu wa Madina kwa miaka kadhaa na ameandika Qur'ani nzima mara kadhaa kwa visomo tofauti.