Main Title

source : Parstoday
Alhamisi

29 Februari 2024

20:54:30
1441295

Uthman Taha atambulishwa shakhsia bora wa mwaka wa Qur'ani

Idara ya Haram ya Imam Hussein bin Ali bin Abi Twalib (as) katika mji mtakatifu wa Karbala, imetoa heshima maalumu kwa Uthman Taha, kwa kumtangaza mwandishi huyu maarufu wa kaligrafia kama shkhsia bora zaidi wa Qur'ani ya mwaka huu.

Sheikh Uthman Husayn Taha anayejulikana zaidi kwa jina la "Uthman Taha" alikamilisha uandishi wa nakala ya Qur'ani kwa maandishi ya Naskh katika miaka ya 1970, na nakala ya Qur'ani aliyoiandika iliwavutia Waislamu wengi kwa miaka mingi.

Uthman Taha ambaye ni mzaliwa wa Syria amekuwa akiishi katika mji mtakatifu wa Madina kwa miaka kadhaa na ameandika Qur'ani nzima mara kadhaa kwa visomo tofauti.