Televisheni ya al Jazeera ya Qatar imeripoti kuwa, Madeleine Dean, mwakilishi wa Kongresi ya Marekani ambaye hivi karibuni alisafiri katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina (Israel) ameongeza kuwa, mashambulizi ya utawala wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza ni makubwa zaidi kuliko inavyoakisiwa kwenye vyombo vya habari.
Mjumbe huyo wa chama cha Democratic katika Baraza la Wawakilishi la Marekani amesema kuwa ukosefu wa uaminifu wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, ukiukaji wa ahadi yake ya kutoshambulia raia na madai ya uongo kuhusu kutengwa maeneo salama huko Gaza, havikubaliki.