Main Title

source : Parstoday
Alhamisi

29 Februari 2024

20:59:42
1441304

Baada ya kutembelea Israel, mbunge wa Kongresi asema: Netanyahu ni kidhabu

Mjumbe wa chama cha Democratic katika Baraza la Wawakilishi la Marekani amepinga mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na Israel huko Palestina na kumtaja Waziri Mkuu wa utawala huo ghasibu kuwa ni mhalifu na mwongo.

Televisheni ya al Jazeera ya Qatar imeripoti kuwa, Madeleine Dean, mwakilishi wa Kongresi ya Marekani ambaye hivi karibuni alisafiri katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina (Israel) ameongeza kuwa, mashambulizi ya utawala wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza ni makubwa zaidi kuliko inavyoakisiwa kwenye vyombo vya habari.

Mjumbe huyo wa chama cha Democratic katika Baraza la Wawakilishi la Marekani amesema kuwa ukosefu wa uaminifu wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, ukiukaji wa ahadi yake ya kutoshambulia raia na madai ya uongo kuhusu kutengwa maeneo salama huko Gaza, havikubaliki.