Main Title

source : Parstoday
Jumamosi

2 Machi 2024

09:40:48
1441606

Khatibu wa Sala ya Ijumaa: Katiba imepelekea kuongezeka ushiriki wa wananchi katika muundo wa kisiasa wa nchi

Imamu wa muda na Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesema juhudi za kutekeleza katiba ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa umakini zaidi kadiri iwezekanavyo ni moja ya sababu kuu za kuongezeka kiwango cha ushiriki na kupanda nafasi na mchango wa wananchi katika mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Wanachuo wa Iran (ISNA), Hujjatul-Islam wal-Muslimin Mohammad Hassan Abu Turabi-Fard, ameeleza katika khutba za Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran kwamba: kuinua kiwango cha ushiriki wa wasomi katika upitishaji maamuzi ya msingi, kurasimisha utawala wa sheria, kuwepo usimamizi wa wananchi juu ya madaraka, kupunguza kiwango cha uendeshaji mambo kupitia Serikali na kueneza utamaduni wa utoaji nafasi kwa wenye sifa kunapunguza mitafaruku na kuwafanya watu wawe wachangamfu katika masuala ya kijamii na huongeza kiwango cha motisha, matumaini na ushiriki wao katika mambo.

Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran ameeleza kuwa, umoja wa kitaifa na mshikamano wa Kiislamu ni stratijia na mikakati miwili isiyo na shaka ya kuimarisha mihimili ya mamlaka ya kitaifa na kugeuza vitisho kuwa fursa na akaongeza kuwa: taifa lenye umoja ni nembo ya azma, irada, matumaini na matarajio ya juu.

Abu Turabi-Fard ameendelea kubainisha kwamba: katika utawala uliotokana na matakwa ya wananchi na unaosimamia misingi ya sheria, mfungamano wa karibu na ulioshikamana wa raia katika uendeshaji wa nchi na uundaji wa taasisi na mifumo ya kisiasa ni miongoni mwa nguzo muhimu zaidi za demokrasia ya kidini na mamlaka ya kitaifa.../

342/