Mchakato wa kuhesabu kura ulianza mara tu baada ya kumalizika zoezi la upigaji kura. Baadhi ya majimbo ya uchaguzi wa Iran uliofanyika jana matokeo yake yameanza kutangazwa.
Kwa mujibu wa ripoti, zaidi ya waandishi 350 kutoka vyombo vya habari 160 na nchi 20 waliripoti uchaguzi wa jana wa duru ya 12 ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge) na Baraza la Wataalamu Wanaomchagua Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Uchaguzi wa duru ya 12 ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge) na Baraza la Wataalamu Wanaomchagua Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ulifanyika jana Ijumaa kote nchini ambapo wagombea wanawania viti 290 vya Bunge na 88 vya Baraza la Wataalamu Wanaomchagua Kiongozi Mkuu wa nchi.
Zaidi ya wagombea 15,200 wanawania viti 290 vya ubunge, 30 kati ya hivyo ni vya mji mkuu, Tehran, ambao unatambuliwa kuwa jimbo kubwa zaidi la uchaguzi nchini. Wabunge hao huhudumu kwa kipindi cha miaka minne.