Kwa mujibu wa IRNA, Rais Raisi, amesema hayo katika mkutano na waandishi wa habari mjini Algiers aliofanya pamoja na mwenyeji wake Rais Abdel Majid Taboun wa Algeria, ambapo sambamba na kuipongeza serikali ya nchi hiyo kwa kuendesha kwa mafanikio Mkutano wa saba wa Baraza la Viongozi wa Nchi Zinazouza Gesi kwa wingi duniani, amesema uhusiano wa Iran na Algeria unakwenda mbali zaidi ya uhusiano wa kisiasa kwa sababu unatokana na mafungamano ya karibu mno katika nyuga za dini, utamaduni na ustaarabu. Rais wa Iran amewaenzi pia mashahidi wa mapambano ya Algeria dhidi ya ukoloni na akasema: "tunawaheshimu Mujahidina wote waliouawa shahidi, ambao walisimama dhidi ya wakoloni kwa istiqama na uvumilivu na uaminifu kwa Uislamu na nchi, na tunaziombea amani roho zao safi".Sayyid Ebrahim Raisi amegusia misimamo ya pamoja ya kisiasa ya Iran na Algeria hususan katika kutetea haki za wananchi madhulumu wa Palestina na kupinga jinai na ukaliaji ardhi kwa mabavu unaofanywa na utawala wa Kizayuni na akasema: kinachojiri leo Ghaza ni mauaji ya kimbari na uhalifu wa kivita, na chimbuko la jinai hiyo linarejea kwenye historia ya miaka 75 ya uvamizi na ukaliaji ardhi kwa mabavu unaofanywa na Wazayuni.
source : Parstoday
Jumatatu
4 Machi 2024
19:57:11
1442205
Raisi: Chimbuko la jinai za Wazayuni Ghaza linarejea kwenye miaka 75 ya uvamizi wao
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, kinachojiri leo Ghaza ni mauaji ya kimbari na uhalifu wa kivita, na chimbuko la jinai hiyo linarejea kwenye historia ya miaka 75 ya uvamizi na ukaliaji ardhi kwa mabavu unaofanywa na Wazayuni.