Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ameyasema hayo leo katika mkutano na Mkuu na wajumbe wa Baraza la Wanazuoni Wataalamu wanaomchagua Kiongozi Mkuu.Akibainisha mantiki hiyo ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kusimama imara na kukabiliana na watumiaji mabavu, Ayatullah Khamenei amesema: hadi kabla ya kuasisiwa Jamhuri ya Kiislamu, kambi pekee iliyokuwepo duniani ilikuwa ni ya demokrasia zenye mfungamano na demokrasia ya kiliberali ya Magharibi, lakini baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu, iliundwa kambi mpya ya mfumo wa Kiislamu unaoendana na ridhaa ya wananchi, ambayo kimsingi ulisimama kukabiliana na demokrasia ya Magharibi.Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kujitokeza kwa kigezo cha Mfumo wa Kiislamu unaotokana na ridhaa ya wananchi nchini Iran kulihatarisha maslahi ya kambi ya demokrasia ya Magharibi na kuanza mizozo na upinzani wa kila mara wa mfumo huo dhidi ya Mfumo wa Kiislamu na akaongezea kwa kusema: sababu ya wao kuhisi hatari hiyo na kuanzisha upinzani wao ni kwamba katika dhati ya mfumo wa demokrasia ya Magharibi kuna hulka ya kiburi, uchokozi, uporaji wa haki za mataifa na kuzusha vita na umwagaji damu usio na kikomo ili kunyakua madaraka; na ushahidi wa hayo ni kukoloniwa nchi nyingi za Asia, Afrika na Amerika ya Kusini katika karne ya 19, yaani, wakati wa kilele cha kauli mbiu na madai yao ya demokrasia, uhuru na haki za binadamu.Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema, dhati ya Kiislamu ndilo suala muhimu zaidi na muelekeo wa kambi ya Mfumo wa Kiislamu unaotokana na ridhaa ya wananchi katika kukabiliana na dhulma na uonevu huo; na katika kujibu suali la kwa nini Jamhuri ya Kiislamu inakabiliana na kambi ya Uistikbari amesema: Iran ya Kiislamu haina ugomvi wowote na nchi, serikali na mataifa, bali inapinga dhulma na uchokozi uliomo ndani ya kambi ya demokrasia ya Magharibi.
source : Parstoday
Alhamisi
7 Machi 2024
14:14:05
1442837
Kiongozi Mkuu: Mantiki ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni ya kusimama imara kukabiliana na kambi ya Uistikbari
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema, mantiki ya kidini, kiakili na ya kiutu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni ya kusimama imara kukabiliana na kambi ya Uistikbari.