Main Title

source : Parstoday
Alhamisi

7 Machi 2024

14:16:41
1442842

Chuki dhidi ya Waislamu zimeongezeka Japan tangu Israel ilipoanza kuishambulia kijeshi Ghaza

Mwanaakademia wa Kijapan, Kayyim Naoki Yamamoto amesema, hisia za chuki dhidi ya Waislamu nchini Japan zinaongezeka tangu utawala haramu wa Kizayuni wa Israel ulipoanzisha vita vya kikatili na mashambulio ya kinyama dhidi ya Ukanda wa Ghaza Oktoba 7, 2023.

Yamamoto, mwanachama wa Taasisi ya Taaluma za Kituruki ya Chuo Kikuu cha Marmara ameeleza kwamba, kumekuwa na ongezeko la chuki dhidi ya Uislamu na Wapalestina katika nchi yake kufuatia mashambulio ya Oktoba 7, 2023. Mwanaakademia huyo amebainisha kuwa, kauli za chuki dhidi ya Waislamu zimeongezeka nchini Japan kutokana na kuongezeka uungaji mkono kwa vyama vya mrengo wa kulia. Yamamoto amesisitiza kwamba chuki dhidi ya wageni (xenophobia), ambazo zimekuwepo kwa miaka mingi katika nchi hiyo ya Asia Mashariki, zimegeuka kuwa chuki dhidi ya Waislamu baada ya mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ghaza.Ameendelea kueleza kwamba hivi sasa Japan inashuhudia mabadiliko hasi ambapo chuki dhidi ya wageni na chuki dhidi ya Waislamu zimeongezeka kwa kasi katika kipindi cha miaka 15 iliyopita.

 Msomi huyo ametahadharisha kwa kusema "Serikali ya Japan haitambui ni balaa la aina gani litasababishwa na kuongezeka hisia za chuki dhidi ya Uislamu". Yamamoto ameeleza pia kwamba chuki dhidi ya Uislamu zimeongezeka zaidi wakati huu nchini Japan kuliko wakati mwingine wowote, na akaongeza kuwa: "Wajapan wanaifuata Marekani kisiasa na kijamii." "Msimamo wa Marekani wa kuunga mkono Israel wakati wa mashambulizi ya Ghaza umesababisha Wajapan kuwa na chuki na Palestina na Uislamu," ameeleza msomo huyo. Kadhalika amesema, Wajapan wanaounga mkono utawala wa Kizayuni wa Israel wameanzisha kampeni dhidi ya Uislamu nchini humo, na kwamba makundi yanayounga mkono utawala huo ghasibu yanaeneza chuki, sio tu dhidi ya Palestina, bali pia dhidi ya nchi nyingine za Kiislamu.../