Main Title

source : Parstoday
Jumamosi

9 Machi 2024

19:50:15
1443270

Iran yataka Israel iondolewe kwenye tume ya Umoja wa Mataifa ya haki za wanawake

Afisa mkuu wa haki za binadamu wa Iran ametoa wito wa kuondolewa utawala haramu wa Israel katika Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya wanawake baada ya maelfu ya wanawake wa Kipalestina kuuawa na kujeruhiwa katika vita vinavyoendelea vya Israel vya mauaji ya kimbari huko Gaza.

Kazem Gharibabadi, Katibu wa Baraza Kuu la Haki za Binadamu la Iran ameyasema hayo katika barua tatu zinazofanana kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Rais wa Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa na Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya haki za binadamu kwa munasaba wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake siku ya Ijumaa.

Akizungumzia uhalifu wa Israel huko Gaza, Gharibabadi amesema "kinachosikitisha zaidi... ni hali ya wanawake na wasichana."

Amebainisha kuwa wanawake na watoto ni asilimia 70 ya waliouawa au kujeruhiwa katika vita vya mauaji ya kimbari vya Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza.

Katika barua zake, Gharibabadi amerejelea ripoti kadhaa za Umoja wa Mataifa zilizofichua athari mbaya ya vita kwa wanawake na wasichana wa Gaza.

342/