Faisal Mekdad amesema hayo katika ujumbe alioutuma kwenye mtandao wa kijamii wa X na kuongeza kuwa, mauaji ya maelfu ya Wapalestina wakiwemo watoto 12,000 yamefichua undumukuwili wa Wamagharibi, ambao wamekuwa wakipiga nara hewa za eti kutetea haki za binadamu duniani.
Waziri Mekdad ameeleza bayana kuwa, "(Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin) Netanyahu ameugeuza Ukanda wa Gaza kuwa magofu, na kusababisha vifo vya watoto zaidi ya 12,000 na wanawake zaidi ya 8,000 Gaza."
Mekdad amesema hatua ya Israel ya kuendelea kufanya mauaji ya kutisha dhidi ya Wapalestina kwa uungaji mkono usio na kifani wa Magharibi imedhihirisha wazi dhati halisi ya kigaidi ya utawala huo na undumakuwili wa nchi za Magharibi.
Idadi ya Wapalestina waliouawa shahidi kufuatia mashambulio ya kinyama ya Israel katika Ukanda wa Gaza tokea Oktoba 7, 2023 mpaka sasa imekaribia 32,000.
342/