Shirika la habari la IRNA limeripoti kuwa, Hossein Amir Abdollahian amesema katika ujumbe wake huo wa pongezi za Ramadhani kwamba matukio ya Gaza yanaonyesha kuwa, suala la Palestina ni lengo la pamoja la Waislamu na ni kadhia kuu miongoni mwa vipaumbele vya Umma wa Kiislamu.
Amir Abdollahian amesema kuwa: Mwezi mtukufu wa Ramadhani unaweza kuwa fursa nzuri kwa nchi za Kiislamu kuchukua hatua madhubuti za kukomesha mauaji ya halaiki na uhalifu wa kivita wa utawala wa kibaguzi wa Israel huko Gaza chini ya mwavuli wa umoja na mshikamano wa pande zote.
Hossein Amir Abdollahian amesema mwishoni mwa ujumbe wake huo kuwa wanamapambano wa Palestina ndio washindi wakuu wa maidani hiyo. Leo Jumanne ni siku ya kwanza ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani hapa nchini Iran na katika nchi kadhaa za Kiislamu kama Indonesia, Malaysia, Australia, Oman, Brunei, Singapore, Iraq na Lebanon. Saudi Arabia, Qatar, Imarati, Lebanon, Palestina, Uturuki na Waislamu wa madhehebu ya Sunni nchini Iraq zilitangaza jana Jumatatu kuwa siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
342/