Kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la Palestina Wafa, walowezi hao wa Kizayuni walivamia Msikiti wa Al-Aqsa kwa makundi kutokea eneo la Babul-Mughaaribah upande wa magharibi wa msikiti huo mtakatifu. Mapema siku ya Jumatatu, walowezi wapatao 275 wa Kiyahudi waliingia kwenye eneo la jengo la Msikiti wa Al-Aqsa kwa wito uliotolewa na makundi ya Kiyahudi yenye chuki na itikadi kali wa kushadidisha hujuma na uvamizi katika msikiti huo wakati wa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
342/