Hussein Amir-Abdollahian ameeleza kuwa, Israel inatekeleza sera hizo ili kutokomeza dalili zote za maisha ya Wapalestina pamoja na utambulisho wao na kuwahamisha wakazi wa eneo hilo kwa nguvu.
Abdollahian amesisitiza kuwa, hii inathibitisha kwamba utawala dhalimu wa Kizayuni unatekeleza kwa makusudi siasa za kuliangamiza kabisa "taifa la Palestina na utambulisho wake."
Abdollahian amesema hayo katika barua aliyoituma kwa Makatibu Wakuu wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC), Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa nchi za Kiislamu ambapo amesema kuhusu matukio ya Palestina kwambna,: Katika hali ambayo inashuhudia kuendelea kutokuwa na uwezo wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa katika kusitisha vita dhidi ya Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan kutokana na Marekani kukwamisha kwa makusudi juhudi za kufikia hilo, kuna haja kwa jamii ya kimataifa kuchukua hatua za dhati za kuwaunga mkono wananchi wa Palestina, kusimamishwa vita haraka na kuliondoa eneo hilo katika hali mbaya ya sasa inalokabiliwa nalo.