Mji huo wa kusini ya Ghaza umekuwa mwenyeji wa kupokea na kutoa hifadhi kwa idadi kubwa ya Wapalestina karibu milioni 2.4 wakazi wa ukanda huo ambao wamekimbilia huko kutokana na janga la vita.
source : Parstoday
Jumapili
17 Machi 2024
20:10:36
1445187
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeutaka kwa msisitizo mkubwa utawala wa Kizayuni wa Israel uchukue uamuzi wa kufuta mpango wake wa kuuvamia na kuushambulia kijeshi kupitia ardhini mji wa Rafah ulioko kusini ya Ukanda wa Ghaza, unaohimili vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendeshwa na utawala huo.