Main Title

source : Parstoday
Jumatano

20 Machi 2024

13:35:41
1445754

Rais Ebrahim Raisi: Mwaka 1403 Hijria Shamsia ni wa kuongeza uzalishaji

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa mkono wa baraka kwa mnasaba wa kuingia mwaka mpya wa Kiirani wa 1403 Hijria Shamsia na kusaidifiana tukio hilo na mwezi mtukufu wa Ramadhani na kusema kuwa, mwaka huu utakuwa wa kuongeza uzalishaji wa bidhaa.

Kwa mujibu wa Iran Press, Sayyid Ebrahim Raisi amesema hayo leo kwenye ujumbe kwa taifa alioutoa kwa njia ya televisheni na kusisitiza kuwa, mwaka huu wa 1403 Hijria Shamsia utakuwa wa ustawi zaidi wa kiuchumi na kupunguza kiwango cha mfumuko wa bei pamoja na kuongeza huduma kubwa zaidi kwa wananchi. 

Raus Raisi amegusia pia njama za maadui za kujaribu kutoa pigo kwa Iran ya Kiislamu na kusisitiza kuwa, mshikamano, umoja na ushirikiano wa wananchi na viongozi ndio ufunguo wa kushinda njama zote za maadui. Amesema, kujitokeza kwa wingi wananchi wa Iran kwenye nyuga za kila namna kunamvunja moyo na kumkatisha tamaa adui. 

Vile vile amegusia matukio ya eneo hili hususan vita vya Ghaza kwenye ujumbe wake huo wa mwaka mpya wa Kiirani wa 1403 Hijria Shamsia na kusema kuwa, muqawama wa kupigiwa mfano wananchi wa Palestina umewalazimisha mabeberu waupe utawala katili wa Israel mabomu ya mabilioni ya dola ili waangamize watu milioni mbili wa Ghaza, lakini wameshindwa.

342/