Kwa mujibu wa shirika la habari la Tasnim, Seyed Ebrahim Raisi, ameyasema hayo katika ujumbe aliowatumia viongozi wa nchi za Kiislamu na kusisitiza kuwa, kuendelea mauaji ya kimbari huko Ghaza na jinai za kivita za utawala wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Palestina bila shaka ndio masuala makuu yanayoshughulisha Umma wa Kiislamu. Amefafanua kuwa, moja ya malengo hatari ya utawala bandia wa Israel ni kufuuta athari zote za maisha na utambulisho wa Wapalestina, kuweka mazingira ya msambaratiko wa kijamii na kiraia na kuwahamisha kwa nguvu wakazi wa Ukanda wa Ghaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan kuelekea nchi jirani. Raisi ameongeza kuwa: utawala wa Kizayuni unatekeleza kwa makusudi sera ya kuliangamiza moja kwa moja taifa la Palestina na utambulisho wake kwa kushirikiana na Marekani.Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, jukumu la kuzuia maafa ya kibinadamu huko Palestina na Ghaza liko mikononi mwa taasisi za kimataifa hususan Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC na Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu na akabainisha kuwa: katika mazingira haya nyeti na hasasi, na katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inatoa indhari juu ya kuendelea ukatili wa mauaji ya wazi kabisa ya kimbari yanayofanywa dhidi ya taifa, na kwa mara nyingine tena inatilia mkazo ulazima wa kuchukuliwa hatua madhubuti na athirifu za kukomesha mauaji hayo, kuondolewa mzingiro kikamilifu na kukabidhiwa kwenye vyombo vya sheria wazayuni watoaji amri na watekelezaji wa jinai zinazofanywa na utawala bandia wa Israel.
Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo, idadi ya Wapalestina waliouawa shahidi kutokana na mashambulio ya kinyama ya jeshi la Israel tangu Oktoba 7 hadi sasa, imeshapindukia 31,923 na waliojeruhiwa pia ni zaidi ya 74,096.../
342/