Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema kuwa uongozi wa Umoja wa Ulaya, unaoipatia Ukraine silaha na kuichochea kutekeleza uhalifu, lazima ubeba dhima sawa na uongozi wa Ukraine kwa vitendo vya kigaidi vinavyofanywa dhidi ya raia wa Russia.
Zakharova amesema katika maoni yaliyochapishwa kwenye tovuti rasmi ya wizara hiyo kwamba "kwa msukumo wa Magharibi, Waukraine hawasiti kufanya vitendo vya kigaidi dhidi ya miundombinu ya kiraia na wakazi wenye amani katika miji ya Russia."Ameongeza kuwa: "Uongozi wa sasa wa Umoja wa Ulaya na nchi wanachama wake, ambazo hutoa misaada ya silaha kwa Kiev na kuichochea kufanya uhalifu wa kimataifa, unapaswa kubeba majukumu na kuwajibishwa pamoja na Ukraine kwa vitendo hivi." Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje Russia amesisitiza kuwa mipango ya Umoja wa Ulaya ya kutenga euro bilioni 50 za msaada wa kifedha na kiuchumi kwa Ukraine "haitauokoa utawala wa Kinazi wa Kiev." Ukraine imepokea msaada mkubwa wa kifedha na kijeshi kutoka nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani, Uingereza, na nchi kubwa za Ulaya, tangu kuanza vita baina ya nchi hiyo na Russia.
342/