Kwa mujibu wa mashuhuda, jeshi la askari katili wa Kizayuni limejiondoa kikamilifu ndani ya hospitali hiyo na vitongoji vinavyoizunguka kuelekea maeneo ya kusini mwa kitongoji cha Tel al-Hawa, kusini magharibi mwa mji wa Ghaza. Mashuhuda hao wameongeza kuwa, katika muda wa majuma mawili wa kuivamia na kuikalia hospitali ya Al-Shifa, vikosi vya jeshi la Kizayuni vilichoma moto majengo yote katika hospitali hiyo na kupelekea kusitishwa utoaji huduma. Imeelezwa pia kwamba, jeshi la Israel limeharibu jengo la upasuaji maalumu na kuchoma moto jengo kuu la mapokezi na huduma za dharura. Vilevile askari katili wa utawala wa Kizayuni wamechoma moto majengo ya wodi za figo na wajawazito, mafriji ya kuhifadhia maiti, na vifaa vya matibabu ya kansa na majeraha ya kuungua, mbali na kubomoa jengo la kliniki ya wagonjwa wa nje.Kulingana na duru za tiba za Palestina, hospitali hiyo kwa sasa haitumiki kabisa kutokana na jeshi la Kizayuni kuharibu vifaa vyote vya matibabu katika vyumba vya wagonjwa, vyumba vya upasuaji na vyumba vya wagonjwa mahututi.
342/