Gazeti la Israel la Haaretz limekusanya na kuchapisha ushuhuda uliotolewa na maafisa na askari wa jeshi la Kizayuni ambao wamepigana huko Ghaza katika vita ambavyo vimekuwa vikiendelea tangu Oktoba 7, 2023. Ripoti ya gazeti hilo imeeleza kwamba: "jeshi la Israel linasema, magaidi 9,000 wameuawa tangu vilipoanza vita vya Ghaza". Hata hivyo, maafisa na wanajeshi wa Israel wameliambia Haaretz kwamba "mara nyingi hawa huwa ni raia ambao uhalifu pekee waliofanya ulikuwa ni kuvuka mstari usioonekana, uliochorwa na jeshi la Israel". Askari mmoja ameliambia gazeti hilo: "tuliambiwa wazi kwamba hata ikiwa mshukiwa anaingia kwenye jengo lenye watu ndani yake, tunapaswa kufyatua risasi kwenye jengo hilo na kumuua gaidi, hata ikiwa watu wengine watajeruhiwa".Kwa mujibu wa ushuhuda wa maafisa na askari wa Kizayuni, jeshi la Israel hufyatua risasi kwa mtu yeyote anayeingia katika lililoainishwa kuwa "eneo la mauaji", awe mtu mwenye silaha au raia.
342/