Main Title

source : Parstoday
Jumanne

2 Aprili 2024

14:39:53
1448526

Balozi wa Iran Syria: Tutajibu mapigo kwa Israel sawa na ilivyoshambulia ubalozi wetu mdogo

Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Syria amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo sawa na utawala wa Kizayuni wa Israel ulivyoshambulia ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria.

Hossein Akbari, balozi wa Iran mjini Damascus ameandika katika mtandao wa kijamii wa X kwamba utawala wa Kizayuni wa Israel ulishambulia kinyama sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria na kinyume na mikataba yote ya kimataifa na kuwalenga waambata rasmi wa kijeshi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.Kufuatia shambulio hilo la kigaidi lililofanywa na utawala wa Israel katika sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus na kupelekea kuuawa shahidi baadhi ya washauri rasmi wa kijeshi wa Iran, balozi mdogo wa Uswisi mjini Tehran ameitwa Wizara ya Mambo ya Nje akiwa msimamiaji wa maslahi ya Marekani nchini Iran, na kubainishiwa ukubwa wa shambulio la kigaidi na jinai hiyo iliyofanywa na utawala wa Israel ikisisitizwa kuwa serikali ya Marekani ndiyo inayobeba dhima hiyo.Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian, salamu muhimu zimetumwa kwa serikali ya Marekani ikiwa ni muungaji mkono wa utawala wa Kizayuni, na Washington itapaswa kuwajibika.

Katika mazungumzo ya simu na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC, Hossein Ebrahim Taha, mkuu wa vyombo vya kidiplomasia vya Iran ametaka jumuiya hiyo ichukue hatua na kutoa mjibizo mwafaka na wa haraka dhidi ya mashambulizi ya kigaidi ya utawala wa Kizayuni katika sehemu ya ubalozi mdogo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Damascus.Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameeleza alivyochukizwa sambamba na kulaani shambulio la kijinai la utawala wa Kizayuni dhidi ya vituo vya kidiplomasia vya Iran, ambalo ni kinyume na kanuni zote za sheria za kimataifa na Mkataba wa Haki za Kidiplomasia na Kibalozi na kusisitizia udharura wa kuchukuliwa hatua na mjibizo mwafaka na wa haraka na OIC dhidi ya jinai hiyo ya utawala wa Israel.../

342/