Main Title

source : Parstoday
Jumanne

2 Aprili 2024

14:40:20
1448527

Shambulio la kigaidi la Israel katika ubalozi mdogo wa Iran Damascus lalaaniwa kimataifa

Russia, Pakistan, Oman, Imarati na Qatar zimeungana na mataifa mengine kuulaani utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kufuatia shambulio la kigaidi ulilofanya utawala huo katika ubalozi mdogo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Damascus, Syria.

Katika shambulio la makombora lililofanywa jana na utawala wa Kizayuni kutokea eneo la Golan unalolikalia kwa mabavu na kulenga ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Jenerali Mohammad Reza Zahedi na Jenerali Mohammad Hadi Haj Rahimi pamoja na watu wengine watano waliokuwa pamoja nao waliuawa shahidi.Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Iran Press, Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imelaani vikali hujuma ya utawala wa Kizayuni dhidi ya jengo la ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus na kuitaka Israel iache vitendo vyake visivyokubalika katika eneo.Mumtaz Zahra, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistan amelaani vikali shambulio la kigaidi la utawala wa Kizayuni katika ubalozi mdogo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Damascus na akalitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lichukue hatua ya kukomesha chokochoko za Israel katika eneo na hatua zake zilizo kinyume cha sheria za kushambulia majirani zake na kulenga vituo vya kidiplomasia vya kigeni. Taarifa ya kulaani shambulio la kigaidi la utawala wa Kizayuni dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus imetolewa pia na Wizara ya Mambo ya Nje ya Oman ambayo imelielezea shambulio hilo kuwa ni ukiukaji wa mamlaka ya kujitawala Syria na sheria zote za ulinzi wa balozi za kidiplomasia.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Muungano wa Falme za Kiarabu, Imarati nayo pia imelaani hujuma ya kigaidi ya utawala wa Kizayuni katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus usiku wa kuamkia leo.Kwa upande wa Qatar, Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo imelaani shambulio la utawala wa Kizayuni dhidi ya jengo la ubalozi mdogo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Syria ikisema ni ukiukaji wa mikataba ya kimataifa na desturi za kidiplomasia. Huku ikitilia mkazo msimamo wake thabiti wa kupinga utumiaji mabavu na ugaidi bila kujali unafanywa kwa sababu gani, Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar kwa mara nyingine imelaani kulengwa vituo vya kidiplomasia na mejengo ya kibalozi .../

342/