Walberg, ambaye aliwahi kuwa mchungaji wa Kanisa amefuta kauli yake hiyo baada ya kukosolewa vikali.Alipokuwa akihutubia mkutano wa watu wa jimbo lake wiki iliyopita, mbunge huyo aliulizwa kuhusu gati ya muda inayojengwa na Marekani karibu na Ghaza kwa ajili ya kupeleka misaada ya kibinadamu kwa watu wa eneo hilo, ambao Umoja wa Mataifa unasema wanakabiliwa na hatari kubwa ya baa la njaa. Katika jibu alilotoa, Walberg alisema: "hatupaswi kutumia hata senti moja kwa misaada ya kibinadamu". Akisema hayo kwenye video iliyowekwa mtandaoni Alkhamisi iliyopita, mbunge huyo aliongeza kuwa: "kila kitu kimalizwe haraka. Iwe vivyo hivyo kuhusiana na Ukraine".Akifafanua zaidi alisema: "inapasa iwe kama Hiroshima na Nagasaki," akimaanisha miji miwili pekee iliyoshambuliwa na Marekani kwa silaha za nyuklia, ambapo watu wapatao 226,000, wengi wao wakiwa raia, walipoteza maisha katika mashambulio hayo mnamo mwaka 1945.
342/