Main Title

source : Parstoday
Jumatano

3 Aprili 2024

20:58:47
1448818

Katibu Mkuu wa UN alaani shambulio la Israel lililolenga ubalozi mdogo wa Iran Damascus

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani shambulio la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria na kuonya kwamba mahesabu yoyote ya kimakosa yanaweza kusababisha mapigano yenye wigo mpana zaidi katika eneo hili tete na lisilo na uthabiti na kusababisha matokeo haribifu kwa raia.

Siku ya Jumatatu, ndege za kivita za utawala wa Kizayuni zilifanya shambulio la anga lililolenga sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran katika Mtaa wa Al-Mazzah mjini Damascus, Syria.Kutokana na uchokozi huo, maafisa saba wa kidiplomasia na waambata wa kijeshi wa Iran waliuawa shahidi.Kwa mujibu wa IRNA, msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric alisema jana kuwa Katibu Mkuu wa umoja huo Antonio Guterres amelaani shambulio la Aprili Mosi dhidi ya vituo vya kidiplomasia vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Damascus pamoja na vifo vilivyoripotiwa. Dujarric amefafanua kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anasisitiza kwamba kanuni ya kinga ya majengo ya kidiplomasia na maafisa wa kibalozi lazima iheshimiwe katika hali zote kwa mujibu wa sheria za kimataifa.Msemaji wa Umoja wa Mataifa ameongeza kuwa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa vilevile anakumbusha pande zote kuheshimu majukumu yao yote chini ya sheria za kimataifa, ikiwa ni pamoja na sheria za kimataifa za kibinadamu.

Kwa mujibu wa Dujarric, "Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anaonya kwamba makosa yoyote ya kimahesabu yanaweza kusababisha mapigano yenye wigo mpana zaidi katika eneo hili tete na lisilo na uthabiti na kusababisha matokeo haribifu kwa raia, ambao kwa sasa wanashuhudia mateso yasiyo na mfano katika nchi za Syria, Lebanon, maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu na Asia Magharibi".Kufuatia shambulio la kigaidi la lililofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limelandikia barua Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ikilitaka lilaani kitendo hicho cha jinai kwa njia kali kabisa na kufanya kikao cha dharura cha kuchunguza ukiukaji wa wazi wa taratibu na misingi ya sheria za kimataifa unaofanywa na utawala wa Israel.Mwakilishi wa Russia katika Umoja wa Mataifa naye pia ametaka kiitwishwe kikao cha dharura chaa Baraza la Usalama, ambacho kilipangwa kufanyika jana Jumanne kwa saa za New York.../

342/