Taarifa iliyotolewa na jeshi la Kizayuni IDF imesema, kulingana na tathmini ya hali ya mambo, imeamuliwa kuwa likizo itasitishwa kwa muda, kwa vitengo vyote vya kivita vya jeshi hilo. Taarifa hiyo imeongeza kuwa, jeshi hilo liko vitani na suala la kutumwa vikosi kwenye medani ya mapigano linapitiwa mara kwa mara inapohitajika. Itakumbukwa kuwa maafisa wa saba wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran IRGC wakiwemo majenerali wawili wakuu, waliuawa shahidi katika shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus siku ya Jumatatu.Iran imeishutumu Israel kwa kutekeleza shambulizi hilo na kuahidi kujibu mapigo.
342/