Kwa mujibu wa gazeti la Irish Times, wanasheria hao wameeleza katika barua ya wazi waliyomwandikia waziri mkuu wa Uingereza Rishi Sunak: "wakati tunakaribisha wito unaozidi kuwa na uzito unaotolewa na serikali yako wa kusitishwa mapigano na kuingizwa misaada ya kibinadamu Ghaza bila kizuizi; wakati huo huo, kuendeleza uuzaji wa silaha na mifumo ya silaha kwa Israel na kukazania kutoa vitisho vya kusimamisha msaada wa Uingereza kwa UNRWA kunazidi kuifanya serikali yako ikwepe kutekeleza sheria za kimataifa”. Barua hiyo imeashiria indhari ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kwamba kuna hatari kubwa ya uwezekano wa Israel kufanya mauaji ya kimbari huko Ghaza na kueleza kwamba: "ni lazima Uingereza ichukue hatua za haraka kukomesha kwa njia za kisheria vitendo vinavyosababisha hatari kubwa ya kufanywa mauaji ya kimbari".Sehemu nyingine ya barua hiyo imesema, kushindwa Uingereza kutekeleza majukumu yake kulingana na mkataba wa mauaji ya kimbari kwa kutochukua hatua zote zilizo ndani ya uwezo wake za kuzuia mauaji ya halaiki kutaibebesha serikali hiyo dhima ya kufanya makosa ya kimataifa, ambayo yatalazimu kulipiwa fidia kamili.
342/