Main Title

source : Parstoday
Jumapili

7 Aprili 2024

14:37:05
1449775

Wapiganaji wa HAMAS waangamiza askari na maafisa 14 wa jeshi la Israel katika muda wa saa chache

Wapiganaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS wamewaangamiza askari na maafisa 14 wa jeshi la Israel katika muda wa saa chache, baada ya kuwashambulia wanajeshi walioko kusini mwa Ukanda wa Ghaza unaohimili vita vya kinyama vya mauaji ya kimbari yanayoendelezwa na jeshi hilo la Kizayuni katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa Mtandao wa Habari wa Muqawama katika Telegram, askari hao wa Kizayuni waliangamizwa jana Jumamosi kwenye msururu wa mashambulizi ya kuvizia yaliyofanywa na tawi la kijeshi la Hamas la Izzuddinul-Qassam katika mji wa Khan Younis. Mashambulizi yaliyoratibiwa kwa umakini zaidi yalifanyika dhidi ya vikosi vya Kizayuni katika kitongoji cha al-Zana na kupelekea kuangamizwa askari tisa. Kwa mujibu wa chaneli hiyo ya habari, operesheni hiyo ilishuhudia wapiganaji wa Kipalestina wakivilenga vifaru vitatu vya Merkava moja kwa moja, na kisha kuwazingira na kuwashambulia kwa vifaa vitatu vya miripuko askari waliokuja kujaribu kuwaokoa wale waliokuwa wamejeruhiwa katika shambulio la kwanza."Vikosi vya uokoaji vililengwa tena saa chache baadaye, pamoja na wale waliokimbilia nyumba iliyo karibu," imeeleza chaneli hiyo ya habari ya Muqawama wa Palestina.

 Ripoti zimeendelea kueleza kwamba: "baada ya kuingia Khan Younis tangu siku 120 zilizopita, vikosi vamizi vya Israel vya IOF vimeshindwa kabisa kufikia malengo yake, vikiendelea kunasa kwenye mtego wa kuviziwa na kuzingirwa na kushindwa kumpata hata mateka mmoja akiwa hai. Muqawama kwa upande wake unaendelea kusubiri mawindo yake yanayofuata". Utawala haramu wa Kizayuni wa Israel ulianzisha vita vya kinyama dhidi ya Ukanda wa Ghaza tarehe 7 Oktoba mwaka jana ili kukabiliana na Kimbunga cha Al-Aqsa, operesheni ya kushtukiza ya kulipiza kisasi iliyotekelezwa na harakati za Muqawama za Ghaza na kupelekea mamia ya Wazayuni kukamatwa mateka. Utawala wa Kizayuni hadi sasa umeshaua Wapalestina wapatao 33,200, wengi wao wakiwa wanawake, watoto na vijana, na kuwajeruhi wengine zaidi ya 75,800.../


342/