Kwa mujibu wa Habib Reza Arzani, Muambata wa Utamaduni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Malaysia, Kongamano la Kimbunga cha Al-Aqsa: Mwamko wa Kibinadamu limefanyika kwa ushirikiano wa Jumuia ya Kimataifa ya Kukuribisha pamoja Madhehebu ya Kiislamu, Kitengo cha Kiutamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mashirika ya Ushauri ya Jumuia za wananchi za Malaysia, Taasisi za Kiutafiti za Kiislamu na Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa Malaysia, na limedhihirisha uungaji mkono mkubwa wa Waislamu wa Malaysia na eneo zima la Kusini mashariki mwa Asia kwa wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina, hasa Gaza. Kuwepo kwa Seyed Ibrahim Seyed Nuh, Mjumbe wa Jumuiya ya Chama cha Palestina katika Bunge la Malaysia, na Mohammed Azmi Abdul Hamid, Mkuu wa Baraza la Ushauri la Kiislamu la Malaysia katika mkutano huo pia kunaonyesha uungaji mkono wa kiwango cha juu kwa masuala ya Palestina na hasa Gaza katika serikali na bunge la nchi hiyo.
Wazungumzaji katika kongamano hilo sambamba na kulaani jinai za utawala ghasibu wa Kizayuni walitilia mkazo zaidi nukta kadhaa muhimu ambazo ni kusimamishwa mashambulizi ya kinyama ya Wazayuni dhidi ya wananchi wasiokuwa na hatia wa Palestina hususan wa Gaza na kuondola mzingiro wa ukanda wa Ghaza ili kurahisisha ufikishwaji misaada ya kibinadamu, kuimarisha umoja wa Waislamu duniani kuhusiana na Gaza, kususiwa bidhaa za Israel na kusimamishwa uhusiano wa aina yoyote ile wa kisiasa na Israel.
Ijapokuwa nchi za Magharibi zimekuwa zikizuia kusimamishwa vita vya Gaza kwa uungaji mkono wao kwa utawala dhalimu wa Kizayuni, lakini mashinikizo ya waliowengi ulimwenguni yamepelekea kutofikiwa malengo ya utawala huo na waungaji mkono wake huko Ghaza. Ali Zahedi, Mtaalamu wa masuala ya kisiasa anasema kuhusiana na hilo: "Uungaji mkono wa kimataifa kwa watu wa Ghaza umepelekea kufeli utawala wa Kizayuni na kubanwa zaidi utekelezaji wa njama zake na wa waitifaki wake katika uwanja huo.
342/