Main Title

source : Parstoday
Jumapili

14 Aprili 2024

19:28:47
1451291

Uamuzi wa Pakistan dhidi ya harakati ya Zainabiyyun; malengo na matokeo yake

Serikali ya Pakistan imechukua uamuzi wa kushtukiza na uliowashangaza na kuwapiga butwaa watu wengi, nao ni wa kuiweka harakati ya Zainabiyyun kwenye orodha yake ya tasisi za kigaidi licha ya kwamba harakati hiyo muda wote imekuwa ikipigania amani na usalama kwa Pakistan.

Tunapoangalia historia ya hadi hivi sasa na harakati ya Zainabiyyun tutaona kuwa, kamwe haijawahi kuchukua hatua yoyote ya kuhatarisha usalama na amani kwenye eneo hili ikiwemo Pakistan, bali katika kipindi cha muongo mmoja cha kuasisiwa kwake, muda wote imekuwa ikipigania usalama wa eneo hili zima. Zainabiyyun inaendesha harakati zake nchini Syria na lengo lake ni kupambana na genge la kigaidi la Daesh (ISIS) na imepata mafanikio makubwa sana katika suala hilo.

Baada ya magenge ya kigaidi kuivamia ardhi ya Syria kutoka kila kona ya dunia, vijana wa Pakistan walijikusanya pamoja na kuanzisha taasisi ya Zainabiyyun kwa ajili ya kwenda kulinda maeneo matakatifu huko Syria. Muongo mmoja umepita tangu taasisi hiyo ianzishwe na muda wote imekuwa ikitangaza hadharani kwamba lengo lake ni kukabiliana na magenge ya kigaidi tena nchini Syria. 

Taasisi hiyo iliasisiwa ikiwa na wanachama 24 tu. Baada ya hapo vijana mbalimbali walijitokeza kujiunga nayo na hivi sasa inajulikana kwa jina maarufu la Jeshi la Zainabiyyun. Harakati hiyo imeshiriki kwenye operesheni mbalimbali kama za ukombozi wa Halab, Nubl na Al Zahraa, Tadmur, Hama na maeneo ya kwenye viunga vya mjini mkuu wa Syria, Damascus. Hata baada ya kukombolewa maeneo hayo, kikosi cha Zainabiyyun kimekuwa na mchango mkubwa katika juhudi za kurejesha hali ya mambo kuwa ya kawaida kwenye maeneo hayo. Wanamapambano wa Zainabiyyun walikuwa mstari wa mbele na ngao imara kwenye operesheni ya Boukamal iliyoongozwa na Luteni Jenerali Qassem Soleimani, operesheni ambayo ilipelekea kuangamizwa na kufutwa kabisa genge la Daesh katika eneo hilo la nchini Syria.

Ali Zahedi, mtaalamu wa masuala ya kisiasa anasema: Vikosi vya wapiganaji kama cha Zainabiyyun viliingia kupambana na magaidi wa Daesh huko Syria baada ya genge hilo kukua na kugeuka kirusi na donda la kensa ambalo lilikuwa linahatarisha usalama wa dunia nzima. Lau kama vikosi kama hivyo vya kujitolea visingelikuwepo, hivi sasa magaidi wa ISIS wangekuwa wana nguvu kwenye eneo hili mpaka Pakistan kwenyewe. Hasa kwa kutilia maanani pia kwamba hata hivi sasa bado mabaki ya magaidi wa Daesh yanafanya vitendo vya kigaidi ndani ya Pakistan, na serikali ya nchi hiyo inalazimika kutumia nguvu za ziada kukabiliana nayo.

Walichokitarajia wananchi wa Pakistan ni kuona serikali yao na jeshi la nchi hiyo linatumia vizuri uzoefu wa wapiganaji wa Zainabiyyun katika kukabiliana na magaidi wa Daesh ndani ya Pakistan na sio kufanya kinyume kabisa na ilivyotarajiwa na kila mtu. Muhimu zaidi kuliko yote ni kwamba harakati ya Zainabiyyun haijawahi kufanya kitendo chochote cha kuhatarisha usalama wa eneo hili na si Pakistan pekee; bali muda wote inapigania kuweko usalama, utulivu na amani katika eneo hili zima.


342/