Ofisi ya Vyombo vya Habari ya serikali ya Ghaza imetoa taarifa maalumu ikielezea kwa kina mashambulio ya siku 190 yaliyofanywa na jeshi la Kizayuni huko Ghaza. Taarifa hiyo imesema, jeshi la Israel limefanya "mauaji 2,973 katika Ukanda wa Ghaza tangu Oktoba 7, 2023."Kwa mujibu wa ripoti ya taarifa hiyo katika mashambulizi hayo ya kinyama yaliyofanywa na jeshi la utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza, watoto 14,560 na wanawake 9,582 wameuawa shahidi.Mbali na hayo, watu 7,000 wamekwama chini ya vifusi au hawajulikani waliko, huku hospitali zikipokea jumla ya watu 33,686 waliouawa na 76,309 waliojeruhiwa.
342/