Naibu Kamishna wa Polisi Nushki Habibullah Mosakhel amewaambia waandishi wa habari kuwa, matukio hayo yamejiri katika wilaya ya mbali ya jimbo la Baluchistan kusini magharibi mwa nchi, wakati watu wenye silaha wasiojulikana walipofunga barabara kuu inayounganisha Pakistan na Iran na kuwaua abiria hao. Kwa mujibu wa Mosakhel, katika tukio la kwanza, watu hao wenye silaha walilizuia gari moja na kuwateka nyara abiria tisa wengi wao wakiwa vibarua, baada ya kuangalia utambulisho wao na kwenda nao kwenye eneo la milima ya jirani. Watu wote hao tisa waliotekwa nyara baadaye walipigwa risasi na kuuawa na miili yao ikatupwa karibu na daraja. Imeelezwa kuwa, marehemu hao wanatokea kaskazini-magharibi mwa Punjab, jimbo kubwa zaidi nchini Pakistan.Katika tukio jengine tofauti, watu wenye silaha wanaosadikiwa kuwa wa kundi lilelile lilioua vibarua, walilifyatulia risasi basi la abiria ambalo halikusimama na kusababisha vifo vya watu wawili na wengine watano kujeruhiwa.
342/