Main Title

source : Parstoday
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:32:04
1452478

Kupingwa njama za Netanyahu za kutaka kususiwa shughuli za UNRWA ndani ya Baraza la Usalama

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya kikao kujadili shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada kwa Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) kufutia maombi ya Algeria na Jordan.

Ziad Abu Amr mwakilishi wa Palestina katika Umoja wa Mataifa amesema katika kikao cha Baraza la Usalama la UN kilichojadili matukio ya Asia Amagharibi na Palestina kwamba Israel inapasa kushinikizwa ili iache kuwasababishia njaa wananchi wa Palestina na iheshimu kanuni za Umoja wa Mataifa. 

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria alisema katika kikao hicho kwamba: Utawala ghasibu wa Israel unalishambulia shirika la UNRWA kwa sababu unataka kuiangamiza Palestina. 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jordan pia alisema: Israel inatumia njaa kama silaha ya kivita na iinawauwa kwa damu baridi wafanyakazi wa mashirika ya misaada ya kibinadamu. Vilevile ametoa wito wa kuhitimishwa uvamizi na kuzikaliai kwa mabavu ardhi za Palestina na kupatikana njia ya ufumbuzi wa kudumuu kwa ajili ya kutatua suala la wakimbzi wa Kipalestina. 

Mwakilishi wa Russia katika Umoja wa Mataifa pia amekosoa mashambulizi na hujuma za kikatili za utawala wa Kizayuni kwa wafanyakazi wa shirika la UNRWA na kusema: Kudhoofishwa nafasi ya shirika hilo kumekuwa na taathira haribifu. 

Mjumbe wa China pia alieleza kuwa hakuna ushahidi wa kuthibitisha madai ya utawala wa Kizayuni kuhusu ushirikiano wa shirika la UNRWA na harakati ya Hamas na kuutaka utawala huo kusitisha mashambulizi yake dhidi ya UNRWA. 

Tangu siku ya kwanza ya kuasisiwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA), utawala wa Kizayuni wa Israel ulijaribu kwa nyakati tofauti kukatisha uhai wa shirika hilo ili kufikia lengo lake la muda mrefu na hivyo kulifanya suala la wakimbizi kutopewa kipaumbele na kuzingatiwa kimataifa.

Aidha mwaka 1982, Ariel Sharon, waziri wa vita wa wakati huo wa Israel, alipanga njama ya kuteka kambi za wakimbizi zinazosimamiwa na shirika la Umoja wa Mataifa la UNRWA ili kuhalalisha uharibifu na jinai dhidi ya raia wa Palestina katika kambi hiyo. Mauaji ya Sabra na Shatila huko Beirut yalitokea wakati washirika wa utawala wa Kizayuni walipoingia katika kambi 2 za wakimbizi na kuwaua kwa umati raia 3,500 wa Kipalestina. Hicho kilikuwa kipindi kigumu zaidi kwa UNRWA. Wakati wa mashambulizi ya kijeshi ya mwaka 2008-2009 dhidi ya Wapalestina huko Gaza, yanayojulikana kwa jina la Operesheni Cast Lead, shule na maghala ya UNRWA yalilipuliwa na utawala wa Kizayuni, jambo ambalo lilizusha wasiwasi mkubwa wa kimataifa. 


342/