Main Title

source : Parstoday
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:35:00
1452483

Mkuu wa UNRWA alaumu vikali hila ya Israel ya kutaka shirika hilo la kusaidia Wapalestina livunjwe

Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na kuwasaidia Wapalestina, UNRWA, Philippe Lazzarini amelaumu vikali kampeni ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kulisambaratisha shirika hilo.

Lazzarini ametoa tamko hilo mbele ya wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa akisisitiza kwa kusema: "leo hii, kampeni ya hila ya kuzima operesheni za UNRWA inaendelea, ikiwa na athari kubwa kwa amani na usalama wa kimataifa".

Lazzarini ameendelea kubainisha kuwa ingawa hali ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza ingali ni mbaya sana lakini UNRWA inajiona inabanwa kutekeleza majukumu yake kutokana na mamlaka za Israel kuinyima nafasi ya kutoa msaada kaskazini mwa Ghaza licha ya amri ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ ya kuongezwa mtiririko wa misaada katika eneo hilo lililowekewa mzingiro.

Mkuu huyo wa UNRWA ameeleza kwamba, mamlaka ya shirika lake yanaungwa mkono na mataifa mengi wanachama wa Baraza la Usalama, hata hivyo shirika hilo linakabiliwa na mashinikizo makubwa.

342/