Main Title

source : abna.ir
Jumanne

21 Aprili 2015

18:12:12
685487

Serikali ya Saudia yaongeza wanajeshi kuishambulia Yemen + picha

Wakati mwezi mzima umefika tangu Saudia arabia kuanza mashambulizi dhidi ya raia wa Yemen bila mafanikio, serikali ya kifalme ya nchi hiyo imepanga kutuma jeshi maalum ili kupambana na wanaharakati wa kishia wa Huthi na kuwalazimisha wananchi wa Yemen kumrudisha madarakani rais Mansoor Hadi.

Wakati mwezi mzima umefika tangu Saudia arabia kuanza mashambulizi dhidi ya raia wa Yemen bila mafanikio, serikali ya kifalme ya nchi hiyo imepanga kutuma jeshi maalum ili kupambana na wanaharakati wa kishia wa Huthi na kuwalazimisha wananchi wa Yemen kumrudisha madarakani rais Mansoor Hadi.

Shambulio  la  anga  lililofanywa  na  muungano  unaoongozwa  na Saudi  Arabia  dhidi  ya  kituo   cha  usalama  kinachoshikiliwa  na wanaharakati wa kishia wa Huthi kaskazini magharibi  ya  Yemen  limesababisha vifo vya  raia wasioa na hatia takriban 25. Watu  waliouwawa walikuwa  wakiishi katika jengo karibu  na  kituo  hicho  cha  usalama ambacho  ndio kilicholengwa.

Nae mfalme  wa  Saudi  Arabia  Salman  leo ameamuru  jeshi  la ulinzi  wa taifa , ambalo  linatambulika  kuwa  na  vifaa vya  kisasa zaidi nchini  humo  katika  majeshi  ya ardhini , kushiriki  katika uvamizi wa  Saudi Arabia  dhidi  ya wananchi wa na kuhakikisha kwamba wananchi hao wanasalimu amri na kumrudisha madarakani rais wasiye mtaka.

Operesheni  za  kijeshi  katika  kampeni hiyo hadi  sasa  zimefanywa na  jeshi  la  anga  la  Saudi Arabia  na  jeshi  la  kawaida  nchini humo  ambalo linapata  amri  kutoka  wizara  ya  ulinzi. Jeshi  la  taifa liko  katika  mfumo  tofauti  na  lina  wizara  yake  binafsi.

Hatua hii ya kuliagiza jeshi la taifa inakuja baada ya majeshi ya kawaida ya Saudia arabia kushindwa kuingia mpakani mwa Yemen, ambapo katika majaribio ya kuingia Yemen, Saudia arabia ilipata pigo la kumpoteza Jenerali wake mmoja ambaye aliuawa na wapiganaji wa Yemen.

Wakati  huo  huo shirika  la  kimataifa  la  kuwahudumia  wahamiaji limesema  leo  linasitisha  kwa  muda operesheni  ya  kuwaondoa wageni  kutoka  Yemen  kwasababu  ya  vikwazo  vya  kiusalama vinavyosababishwa  na  pande  zote  zinazohusika  katika  mzozo huo.

IOM  imesema  imewahamisha  zaidi  ya  raia  wa  kigeni  400 kutoka  katika  nchi  hiyo  inayokumbwa  na  vita  tangu  Aprili  12.