Main Title

source : abna.ir
Jumamosi

25 Aprili 2015

11:52:55
686242

Zilzala la sababisha maafa Nepal + Picha

Tetemeko kubwa la ardhi limekumba eneo lililo magharibi mwa Nepal.

  Tetemeko kubwa la ardhi limekumba eneo lililo magharibi mwa Nepal.

Shirika la utafiti la Marekani liliseme kuwa tetemeko hilo la vipimo vya 7.9 lilikumba eneo lililo umbali wa kilomita nane mashariki mwa Pokhara magharibi mwa mji mkuu wa Kathmandu.

Kuna ripoti za uharibifu wa majengo. Idadi ya watu waliokufa au kujeruhiwa haijulikani.

Picha za majengo yaliyokuwa yameporomoka pamoja na mahekalu ya miaka mingi iliyopita zimeonekana kwenye mitandao ya kijamii.

Mawasiliano ya simu nayo yameharibiwa.

Walioshuhudia walisema kuwa watu walikimbia nje ya majengo muda mfupi baada ya tetemeko hilo kutokea.

  Matetemeko mengine madogo yameripotiwa kutokea kaskazini mwa India pamoja na nchini Pakistan.