Main Title

source : abna.ir
Jumanne

26 Januari 2016

20:36:19
732155

Papa Francis amuomba rais wa Iran asaidie mpango wa amani mashariki ya kati + Picha

Kiongozi wa kanisa Katoliki Papa Francis leo ameiomba serikali ya Jamhuri ya kiislamu ya Iran kuunga mkono juhudi za amani katika mashariki ya kati

Shirika la habari la ABNA linaripoti kuwa: Kiongozi  wa  kanisa  Katoliki Papa  Francis leo ameiomba serikali ya Jamhuri ya kiislamu ya Iran  kuunga  mkono  juhudi  za  amani  katika  mashariki ya  kati,  wakati  taifa  hilo lenye nguvu  ambalo ni  Jamhuri  ya  Kiislamu  linajitoa kutoka  katika  hali  ya  kutengwa  kimataifa  na  kuchukua hatua  muhimu  kusonga  mbele  wakati  wa  ziara  ya kwanza  ya  rais Hassan Rouhani  katika  makao  makuu ya  kanisa  hilo mjini  Vatican.

Baada  ya  kuondolewa  vikwazo  vya  kimataifa vilivyowekwa dhidi  ya  mpango  wa  amani wa nyuklia ya Iran , rais Rouhani alitumia  dakika  40 katika  makao  makuu  ya kanisa Katoliki  Vatican  kwa  mazungumzo  ya  faragha na papa  Francis , muungano  mkono  mkubwa  wa makubaliano  na  Tehran.

Katika  taarifa  baadaye, makao  makuu  ya  kanisa  hilo yamesema  Francis  amemuomba  kiongozi  huyo  wa  Iran kutumia ushawishi  muhimu  wa  Iran  kuhimiza, pamoja  na nchi  nyingine , suluhisho linalofaa  la  kisiasa , katika matatizo yanayolikumba  eneo  la  mashariki  ya  kati   na kusaidia  kupambana  na  ugaidi  na  biashara  ya  silaha.

Jamhuri ya kiislamu ya Iran ni nchi inayoongozwa kwa misingi ya kiislamu na ina msaada mkubwa katika kupambana na magaidi wanaodhaminiwa na Saudia arabia mashariki ya kati.

Mwisho wa habari/ 291