Main Title

source : abna.ir
Jumanne

26 Januari 2016

20:48:02
732156

Majeshi ya Syria yaukamata mji muhimu Sheikh Miskeen baada ya kuwaangamiza magaidi + Picha

Milio ya mabomu na risasi ilitanda anga la mji huo, huku magaidi wakionekana wakilazimika kukimbia na kiacha asasi na vifaa vyao nyuma huku wengine wengi wakiwa wamekufa na wengine wamejeruhiwa.

Shirika la habari la ABNA linaripoti kuwa: majeshi ya utawala  halali wa  Syria  yaumekamata  mji  muhimu  upande wa kusini  kutoka mikononi   mwa magaidi wanaodhaminiwa na Marekani na Saudia arabia, wakati  muungano  mkuu  wa upinzani  unatarajiwa  kujadili iwapo ushiriki  katika mazungumzo  ya  amani  mjini  Geneva  wiki  ijayo ama  lah .

Kukamatwa  kwa  mji  wa  Sheikh Miskeen katika  jimbo  la kusini  la  Daraa ni  ushindi  mkubwa wa  hivi  karibuni  kabisa  wa majeshi  ya  serikali, ambayo  yamekuwa  yakisonga  mbele tangu  pale  wataalamu wa vita kutoka Iran na majeshi  ya  Urusi na  yalipoanza  mashambulizi ya  anga  nchini  humo  mwishoni  mwa  Septemba.

Milio ya mabomu na risasi ilitanda anga la mji huo, huku magaidi wakionekana wakilazimika kukimbia na kiacha asasi na vifaa vyao nyuma huku wengine wengi wakiwa wamekufa na wengine wamejeruhiwa.

Wakati  huo  huo viongozi  wa  Umoja  wa  mataifa wanaohusika  na  masuala  ya  kiutu  wameziomba  pande zinazopigana  nchini  Syria  kuacha  kuzishambulia  shule, ili  kuruhusu wafanyakazi  wa  kutoa  misaada  kuwafikia wagonjwa na kuepuka kushindwa  kisiasa  kumaliza mzozo huo unaoondelea.

Mratibu wa masuala ya  kiutu  wa  Umoja  wa  Mataifa Yacoub El Hillo amesema  wajumbe  watakaoshiriki mazungumzo watambue  kwamba sasa inatosha.

Amesema watu milioni 4.5 wanaweza  kufikiwa  na  kupata msaada iwapo mashambulizi  ya  kijeshi  yatakoma.

Mwisho wa habari/ 291