-
Kula mweleka njama za Marekani za kuunga mkono mauaji ya kimbari ya Israel kwenye UN
Azimio lililopendekezwa na Marekani la kuunga mkono mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Ghaza limegonga ukuta baada ya kupigiwa kura ya veto na Russia na China ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
The Washington Post: Kauli za Kushner kuhusu Gaza ni dalili ya sera ya baadaye ya Trump
Gazeti la Marekani la The Washington Post limeripoti kuwa muhula wa pili wa Donald Trump, iwapo atashinda uchaguzi ujao wa rais nchini Marekani, "huenda ukamaanisha uungaji mkono mkubwa zaidi wa Washington kwa watawala wa sasa wa Israel wanaotaka kuwafukuza Wapalestina kutoka Gaza na kulikalia tena kwa mabavu eneo hilo."
-
Guterres aonya dhidi ya "sera za kindumakuwili" kuhusu mafaili ya Ukraine na Gaza
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameionya jamii ya kimataifa dhidi ya "sera za kindumakuwili" katika kushughulikia mafaili ya Ukraine na Gaza.