Kwa mujibu wa shirika la habari la kimataifa la AhlulBayt (ABNA), jarida la "Daily Telegraph" katika ripoti yake limesema kuwa Uingereza imelifuta jina la Palestina kwenye ramani zake za kihistoria.
Hatua hii imechukuliwa ili kuitikia ombi la kikundi cha "Wanasheria wa Uingereza Wanaoiunga mkono Israel", na hivyo jina la Palestina limeondolewa kwenye ramani na vibao vya maelekezo katika idara ya Mashariki ya Kati. Hapo awali, katika baadhi ya ramani na vibao vya maelezo kuhusu Misri ya kale na Wafoniki, pwani ya mashariki ya Bahari ya Mediterania ilikuwa imetambuliwa kwa jina la Palestina, na baadhi ya makabila yalikuwa yakielezwa kuwa na "asili ya Palestina".
Your Comment