Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul Bayt (ABNA) – Waziri Msaidizi wa Masuala ya Dini na Upatanisho wa Kidini wa Pakistan alikutana na Balozi wa Uholanzi mjini Islamabad na kuzungumzia kuhusu kuimarisha mazungumzo ya kidini, kulinda haki za walio wachache na ushirikiano wa kikanda.
Katika mkutano huu uliofanyika Jumatano katika afisi ya Waziri mjini Islamabad, pande zote mbili ziliana maoni kuhusu masuala ya manufaa ya pamoja.
Pande mbili zilisisitiza kujitolea kwao kukuza amani, mazungumzo na udugu katika eneo hili na wakaita kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu kuwa moja ya nguzo za ushirikiano wa pamoja.
Waziri wa Masuala ya Dini wa Pakistan katika mkutano huu akirejelea hotuba ya kihistoria ya Muhammad Ali Jinnah ya tarehe 11 Agosti 1947, alibainisha kuwa haki za walio wachache zimefafanuliwa waziwazi katika hotuba hiyo na pia zimehakikishwa katika katiba ya Pakistan.
Aliongeza kuwa wizara yake inaandaa kikamilifu mikutano na mazungumzo ya kidini kote nchini na sherehe za kidini za walio wachache wote huadhimishwa kwa msaada rasmi.
Kwa mujibu wa Kuhistani, katika mfumo wa "Mfuko wa Ustawi wa Walio Wachache", udhamini wa masomo hutolewa kwa watoto wa jamii zisizo za Kiislamu na hatua kubwa zimechukuliwa kwa ajili ya utunzaji na ukarabati wa maeneo ya ibada.
Kwa upande wake, Balozi wa Uholanzi aliielezea Pakistan kuwa nchi ya kipekee yenye utofauti mkubwa wa kidini, kiutamaduni, kijiografia na lugha na akasema nchi yake haina wizara huru ya upatanisho wa kidini na ina nia ya kufaidika na uzoefu wa Pakistan katika eneo hili.
Akisisitiza kuwa serikali ya Uholanzi inaona umuhimu maalum kwa haki za binadamu na inapinga ubaguzi wowote, alisifu juhudi za Pakistan katika kukuza mazungumzo ya kidini na urafiki kati ya jamii mbalimbali.
Your Comment