Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Abna lenye kunukuu kutoka kwenye mtandao wa Al Jazeera, Harakati ya Kiislamu ya Upinzani Hamas ilikitaja kitendo cha walowezi wa Kizayuni kuchoma msikiti katika kijiji cha Tal, magharibi mwa mji wa Nablus, kuwa uhalifu wa kifashisti na uliopangwa na wakielezea kama ukiukaji wa wazi wa maeneo ya ibada na takatifu za Kiislamu.
Katika taarifa yake, Hamas ilisema zaidi kuwa shambulio hili lilifanyika ndani ya mfumo wa uvamizi wa mara kwa mara wa walowezi dhidi ya maeneo matakatifu ya Kiislamu na linaonyesha sera za kimakusudi za kujenga mvutano na ukosefu wa usalama katika ardhi za Palestina.
Harakati hiyo pia iliwaita watu wa Palestina kuchukua hatua za kina, kulinda misikiti na maeneo matakatifu dhidi ya mashambulizi ya walowezi na kukabiliana na uvamizi huu wa mara kwa mara.
Your Comment