12 Machi 2026 - 13:55
Source: ABNA
Ujerumani inasimama upande mbaya wa historia kwa kupuuza uhalifu wa Marekani

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje alisema: Ujerumani inasimama upande mbaya wa historia kwa kupuuza udhalimu na uhalifu wa wavamizi wa Kimarekani na Kizayuni.

Kulingana na shirika la habari la Abna, Ismail Baghaei, msemazi wa Wizara ya Mambo ya Nje, akijibu madai ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani wakati wa safari yake katika maeneo ya Palestina yaliyokaliwa, aliandika ujumbe katika mtandao wa X:
"Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani! Wewe unasimama pamoja na upande wa mvamizi huku ukikataa ukweli kwamba ni utawala wa Israeli ambayo ilishambulia Iran na kuwaua raia wa Iran - pamoja na watoto 168 wasio na hatia katika mji wa Minab.
Hii ni njia inayoweka binadamu upande mbaya wa historia: kupuuza udhalimu na uhalifu wa aibu."

Your Comment

You are replying to: .
captcha